KKKT waanza mchakato wa kumpata mrithi wa Askofu Dk. Fredrick Shoo


Wajumbe wa halmashauri kuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Ijumaa Augusti 23, 2019 watamchagua mkuu wa kanisa hilo atakayeliongoza kwa miaka minne ijayo.

Tayari leo Jumanne Augusti 20, 2019 wajumbe hao wameanza kikao cha ndani ikiwa ni sehemu ya mkutano mkuu wa 20 wa kanisa hilo.

Ikumbukwe Mkuu wa Kanisa hilo hivi sasa, Askofu Dk Fredrick Shoo amemaliza muhula wa kwanza wa miaka minne na wajumbe hao wanaweza kumwongezea muhula wa mwisho au kumchagua mwingine.