https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mamia wazidi kufarikia India kutokana na mafuriko | Muungwana BLOG

Mamia wazidi kufarikia India kutokana na mafuriko


Idadi ya vifo inayotokana na mafuriko yaliyoambatana na dhoruba kali nchini India imefikia watu 154 huku zaidi ya watu milioni moja wakihamishiwa katika kambi za muda.

Kwa mujibu wa maafisa wa kupambana na maafa, hali ya mafuriko bado ni mbaya na vifo vingi vimeripotiwa katika wilaya za Kerala, Wayanad na Malappuram.

Msimu wa dhoruba kali nchini India huwa kati ya mwezi Juni na Septemba ambapo mvua kubwa husababisha uharibifu na vifo.