Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Janeth Magufuli Wameshiriki pamoja na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki Misa Takatifu Dominika ya 18 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam. Ibada iliyoongozwa na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule, Agosti 04,2019.