Wapenzi kutoka Ufaransa wakabiliwa na hukumu ya wizi wa mchanga

Wapenzi kutoka Ufaransa wamekamatwa na kilo 40 za mchanga wa Sardinian katika gari lao na wanaweza kukabiliana na kifungo cha miaka 6 jela.

Walisema kuwa walitaka kuondoka na mchanga nyumbani kwao na hawakujua kama wamefanya makosa.

Ni kosa la jinai kwa mtu kuhamisha mchanga kutoka katika kisiwa cha Sardinia, kwa sababu mchanga unatambulika kama mali ya umma.

Kwa miaka mingi, wakazi wa eneo hilo wamekuwa wakilalamikia wizi wa mali asili ikiwa ni pamoja na mchanga.

Wapenzi hao wanaweza kuhukumiwa kati ya mwaka mmoja jela mpaka miaka sita kwa kosa la wizi wa mali ya umma.

Chini ya sheria ya mwaka 2017, biashara ya mchanga na mapambo ya bahari ni kunyume cha sheria, na faini ya yuro 3000.

Polisi walikuta mchanga umewekwa kwenye chupa 14 ambazo zilitoka katika ufukwe wa Chia , kusini mwa Sardinia katika buti ya gari la wapenzi hao.

Mwaka 1994, ufukwe uliopo kisiwa cha Budeli kaskazini mashariki mwa Sardinia uliwekewa zuio kwa ajili ya siku siku za mbeleni.

Mamlaka ina hofu ya tani kadhaa zinazopotea katika kisiwa hicho kila mwaka.

Watalii, kutoka ulaya wakijumuisha raia wa Italia, huwa wanafanya mnada wa chupa za mchanga mtandaoni.