Yabainika Harry Maguire alikataa Tsh. Milioni 700 akabukuli 500 za Man Utd


Beki Harry Maguire alikataa ofa ya Man City ya mshahara wa Pauni 278,000 (Tsh Mil 776) kwa wiki na kukubali kujiunga na Man United ambapo alisaini mkataba wa miaka sita na mshahara wa Pauni 190,000 (Tsh Milioni 530) kwa wiki, Pauni 88,000 (Tsh Milioni 245) pungufu na ule angepokea Man City.

Kwa mujibu wa gazeti la Uingereza lacDaily Star, endapo Maguire angekubali kwenda City, angepokea jumla ya Pauni Milioni 70 (Tsh Bilioni 195) ndani ya miaka mitano na kuwa beki aliyelipwa zaidi duniani.