Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameeleza sababu za kutenguea uteuzi wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk. Stephen Kebwe.
Amebainisha hayo leo wakati akiwaapisha Viongozi mbalimbali aliowateua Septemba 20 mwaka huu, hafla iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam.
“Mkoa wa Morogoro tulitakiwa tuufanyie Demo tutengue kuanzia Mkuu wa Mkoa hadi Mtendaji wa Kijiji wote halafu tunaweka wapya, aliyekuwa RAS wa pale niliagiza astaafu mapema yeye kazi yake ni kuzungumza na walimu anawatoa Vijijini anawaleta Mjini wale anaozungumza nao vizuri”ameeleza Rais Magufuli.
Ameendelea kwa kusema, "Sasa ukizungumza Mkoa wa Morogoro unagundua RC Kebwe alishindwa kazi, ukipewa Mkoa halafu waliopo chini yako wanafanya mambo ya ajabu maana yake hautoshi, DC na DED wanagombana na haujawahi kusema chochote wala kukemea hautoshi”