Rais Magufuli amtumbua Mkuu wa Mkoa wa Morogoro


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amemteua Lowata Sanare kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, akichukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Stephen Kebwe Ambapo Sanare kwasasa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha.

Akitangaza uteuzi na utenguzi huo leo Septemba 20, 2019 Katibu Mkuu Kiongozi,  Balozi John Kijazi.

Kiongozi huyo ataapishwa Jumapili ya tarehe 22, Septemba, 2019 Ikulu jijini Dar es Salaam.