TANZIA: Omary Nundu afariki dunia


Aliyekuwa mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Mawasiliano ya Simu Tanzania (TTCL) na kisha kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel, Omary Nundu amefariki dunia leo, Jumatano, Septemba 11 jijini Dar es Salaam.

Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi Lugalo.