Walimu Tabora walalamikia utendaji wa benki yao



Na Rahel Nyabali, Tabora.

Baadhi ya walimu mkoani Tabora  wameeleza kupoteza Imani na benki ya walimu nchini MCB  wakidai kutoridhishwa na utendaji wa benki hiyo hasa pale wanapohitaji kuhudumiwa na banki hiyo kama wanachama wake.

Yameelezwa hayo Wakati benki ya walimu nchini MCB ikiwa katika utekelezaji wa kampeni yake iliyopewa jina la Amsha amsha iliyofanyika wilayani Tabora mkoani Tabora  iliyolenga kuwahamasisha walimu walejee kuitumia benki hiyo.


Wakizungumza wakati  wa  kampeni hiyo ya  Amsha  Amsha iliyowakutanisha viongozi wa chama cha Waalimu  ngazi za wilaya  pamoja na baadhi ya  maafisa  kutoka  benki  ya MCB Peter  Sizya  ni Mwalimu  wa shule ya msingi Bombamzinga amesema  ni wakati wa benk kuwajibika ili kufikia malengo yake.


Richard Makungwa ni mkurugenzi mtendaji wa benki ya walimu nchini Sanjali na  kukiri  mapungufu  kadhaa katika benki hiyo ya MCB ametoa wito kwa walimu kushilikiana na benki.


Aidha  mkuu  wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ameitaka  benki ya Walimu nchini MCB kufanya  kazi kwa ushindani ili kuwavutia wateja wengi zaidi.