https://monetag.com/?ref_id=TTIb Wateja wafurahia Intaneti ya bure katika mkutano wa SADC wa Mawaziri wa TEHAMA | Muungwana BLOG

Wateja wafurahia Intaneti ya bure katika mkutano wa SADC wa Mawaziri wa TEHAMA

Ofisa Mawasiliano wa Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Innocent Mungi akipata maelekezo kutoka kwa mfanyakazi wa Tigo juu ya huduma mbalimbali zitolewazo na kampuni hiyo wakati wa mkutano wa mawaziri wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika (Sadc).Kampuni ya Tigo imedhamini mkutano huo kwa kutoa huduma ya intaneti bure.

Mshereheshaji maarufu nchini katika shughuli za kiserikali, Peter Mavunde akipatiwa huduma kutoka kwa wafanyakazi wa kampuni ya Tigo wakati wa Mkutano wa mawaziri wa nchi wananchama wa Sadc.Tigo ni mmoja wa wadhamini wa mkutano huo.

 Katibu wa Mamlaka ya Usafirishaji wa anga Tanzania (TCAA), Vallery Chamulungu akipata huduma kutoka kwa wafanyakazi wa kampuni ya Tigo wakati wa mkutano wa mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc). Kampuni ya Tigo imedhamini huduma ya intaneti bure (Wi-fi).