Habari njema kwa mashabiki wa Liverpool kuelekea kwenye mchezo dhidi ya Manchester United

Klabu ya Liverpool inazidi kupata nguvu baada ya wachezaji wake Alisson Becker na Joel Matip kuanza kurejea kwenye mazoezi kuelekea kwenye mchezo wao wa Ligu kuu dhidi ya Manchester United utakaopigwa Jumapili.

Alisson alikua nje ya dimba baada ya kuumia kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Norwich ambapo Liverpool iliibuka na ushindi wa bao 4-1 katika mechi ya ufunguzi wa msimu.

Wakati Matip aliumia kwenye mchezo dhidi ya Sheffield United ambapo Liverpool ilishinda 1-0 na kukosa michezo dhidi ya FC Salzburg na Leicester City.