https://monetag.com/?ref_id=TTIb Kibarua cha kocha wa Arsenal kipo matatani | Muungwana BLOG

Kibarua cha kocha wa Arsenal kipo matatani


Kibarua cha kocha wa Arsenal, Unai Emery, kipo matatani baada ya mabosi wa timu hiyo kumtaka ahakikishe timu inarudi kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.

Huu ni mwaka wa tatu mfululizo kwa Arsenal kushindwa kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, hivyo wameamua kutumia kiasi kikubwa cha fedha wakati huu kuboresha kikosi hicho, ili waweze kurudi kwenye michuano hiyo mikubwa barani Ulaya.

Kwa mara ya pili mfululizo Arsenal inashiriki michuano ya Kombe la Euro baada ya kushindwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya, huku mashabiki na uongozi wakiwa na kiu ya kutaka kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya.