https://monetag.com/?ref_id=TTIb Utafiti: Huyu ndiye mwanamke mwenye mvuto zaidi duniani | Muungwana BLOG

Utafiti: Huyu ndiye mwanamke mwenye mvuto zaidi duniani


Staa na mwanamitindo, Bella Hadid kutoka nchini Marekani, ametajwa kuwa mwanamke mzuri zaidi duniani kwa mujibu wa utafiti wa kisayansi.

Utafiti huo ujulikanao kama Golden Ratio of Beauty Phi, ambao ni utafiti wa kisayansi unaoonyesha matokeo yaonyeshayo uso mzuri, umemtaja mrembo huyo kuwa ndiye mzuri zaidi akiwapiga chini warembo wengine kama Gigi Hadid, Beyonce, Cara Delevingne na Katy Perry.

Bella, 23 amejibebea taji hilo baada ya kupata 94.35% ya vipimo hivyo na kumfanya mtu aliyekaribia zaidi 100% ya vipimo hivyo ambayo ndio vinatajwa kuonesha sura nzuri.