Waliobambikiwa fedha bandia wahitajika kwa DC Sabaya


Mtandao wa usambazaji wa pesa bandia umeanza kukamatwa katika wilaya ya Hai baada ya mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, kumkamta Mtuhumiwa Richard, akiwa na kiasi cha pesa za Bandia milioni 11.

Mtuhumiwa huyo amekamatwa na fedha hizo katika mji wa Bomang'ombe wakati akijiandaa kuzisambaza.

Hata hivyo mkuu huyo wawilaya ameagiza wananchi wote wa wilaya hiyo walioshikishwa fedha hizo kufika ofisini kwake jumatatu ya tarehe 21 Octoba 2019.