Waziri Kamwelwe ayapongeza Makampuni ya China


Na. Adelina Kapaya

Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mwandisi Izack Kamwelwe ametoa pongezi kwa makampuni  ya kichina, China Railway Seventh Co LTD, Wu Yi Co Ltd  of  China kwa kasi ya ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mpanda Mkoa wa Katavi hadi Mkoa wa Tabora baada ya kufanya ziara ya kushitukiza usiku.

Waziri Kamwelwe amesema amefurahishwa na kasi ya ujenzi wa barabara hio yenye urefu wa kilometa 242 inayojengwa kwa kiwango cha lami na makampuni hayo   mara baada ya kumaliza kukagua barabara hiyo

Alisema licha ya Ujenzi wa barabara hio pia kwa upande wa daraja la Mto Koga  ambalo linaunganisha Mkoa ya Katavi na Tabora ambalo likijaa maji wakati wa masika husababisha barabara hio kufungwa   kufikia mwezi desemba mwaka huu daraja hilo litakua limekamilika na kuanza kutumika

Hata hivyo, Kamwelwe alifanya ukaguzi wa barabara ya kutoka Itigi Mkoani Singida kuelekea Tabora yenye urefu wa kilometa 85 inayojengwa kwa kiwango cha lami na kuridhika na juhudi wanazozifanya kuhakikisha Ujenzi wa barabara unakamilika

Meneja wa Tanroads wa Mkoa wa katavi Mwandisi Martin Mwakabende amesema kutokana na juhudi wanazotumia watahakikisha barabara inakamilika kufikia Desemba mwaka huu na kubaki kazi ya kuweka alama za barabarani ambayo haitachukua mda mrefu kukamilika.

Mwakabende amesema mwezi Desemba mwaka huu mkandalasi wa  kampuni ya kichina China   Rallway   Seventh Co LTD  anatalajia kukabidhi barabara ya kutoka Mpanda kuelekea Uvinza Mkoa wa Kigoma  yenye urefu wa kilimeta 35 iliyojengwa kwa kiwango cha lami ambayo iligharimu kiasi cha shilingi billion  57,871 kwa serikali hadi kukamilika kwa barabara hio.

Li  Wenlon ambaye ni Meneja wa kampuni ya kichina Wu  Yi Co  Ltd   of  China inayotengeneza barabara nyenye urefu wa kilometa 108 kutoka Komanga  hadi  Kasinde Inyonga  kampuni hio imeagiza vifaa vya kutosha kutoka nchi ya Afrika  ya Kusini ili kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa barabara hio kwa kiwango cha lami.