Adama Traore aitwa kwenye kikosi cha Hispania


Adama Traore ameitwa kwenye kikosi cha Hispania kinachojiandaa na mechi za kufuzu Euro2020 ili kuziba pengo la winga Rodrigo Moreno aliyepata majeraha.

Jumanne iliripotiwa winga wa Wolves, Adama Traore amechagua kuitumikia timu ya taifa ya Mali na atakuwepo kwenye mechi za kufuzu AFCON 2021 wikendi ijayo

Traore wazazi wake ni wazawa wa Mali ila yeye kazaliwa Catalonia na amewahi kucheza kwenye timu za vijana za Hispania (Miaka 16,17,19 na 21 ) lakini hajawahi kucheza kwenye timu kubwa, hivyo Traore kazi kwake kuchagua kuitumikia Mali au Spain.