Baridi kali yasababisha safari za ndege kufutwa Marekani

Majimbo ya magharibi na kati ya nchini Marekani yameanza kupata athari za hali ya hewa ya baridi kali.

Mamlaka zimefahamisha kwamba katika majimbo ya Michigan na Kansas ajali za barabarani zilisababishwa na barafu na hali ya hewa ya ubaridi zimesababisha vifo vya watu 4 akiwamo mtoto mmoja.

Kutokana na kunyesha kwa barafu takribani safari za ndege 1200 katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa  O’Hare uliopo katika mji wa Chicago jimbo la Illinois zilifutwa.

Kutokana na barafu zilizokuwapo katika uwanja wa ndege wa O’Hare, ndege moja iliacha njia, hakuna alijyejeruhiwa miongoni mwa abiria 41 waliokuwamo kwenye nege hiyo.

Mamlaka za hali ya hewa zimefahamisha kwamba barafu itaendelea kunyesha katika majimbo ya Indiana, Michaigan na Vermont.