https://monetag.com/?ref_id=TTIb Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson aongoza Semina kuhusu nafasi ya Bunge katika mapinduzi ya Lishe nchini | Muungwana BLOG

Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson aongoza Semina kuhusu nafasi ya Bunge katika mapinduzi ya Lishe nchini

Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiongoza semina kuhusu nafasi ya Bunge katika Mapinduzi ya Lishe nchini iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma. Semina hiyo ilihudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi ya Agri Thamani, Mhe. Mizengo Pinda (kulia kwake), Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge, Kikundi cha Wabunge Vinara wa Lishe, Mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya UKIMWI na Sekretariat ya Kamati ya Uongozi ya Bunge.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi ya Agri Thamani Foundation, Mhe. Mizengo Pinda akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya uongozi, Kikundi cha Wabunge Vinara wa Lishe, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Wajumbe wa Sekretariat ya Kamati ya uongozi ya Bunge kwenye semina kuhusu nafasi ya Bunge katika Mapinduzi ya Lishe nchini iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi ya Agri Thamani Foundation, Mhe. Mizengo Pinda akionyesha kijarida kinachotoa uelewa mpana zaidi wa janga la udumavu na utapiamlo nchini mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge za uongozi, Kikundi cha Wabunge Vinara wa Lishe, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Wajumbe wa Sekretariat ya Kamati ya uongozi ya Bunge kwenye semina kuhusu nafasi ya Bunge katika Mapinduzi ya Lishe nchini iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya uongozi, Kikundi cha Wabunge Vinara wa Lishe, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Wajumbe wa Sekretariat ya Kamati ya uongozi ya Bunge wakiwa kwenye semina kuhusu nafasi ya Bunge katika Mapinduzi ya Lishe nchini iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.

Mkurugenzi Idara ya Elimu ya Lishe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC), Ndg. Sikitu Simon akiwasilisha maada mbele ya Wajumbe Kamati za Kudumu za Bunge za uongozi, Kikundi cha Wabunge Vinara wa Lishe, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Wajumbe wa Sekretariat ya Kamati ya uongozi ya Bunge wakati wa semina kuhusu nafasi ya Bunge katika Mapinduzi ya Lishe nchini iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.

Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kushoto) akizungumza na Viongozi  kutoka Agri thamani Foundation Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Agri Thamani Foundation na Kiongozi wa Msafara, Mhe. Mizengo Pinda, Mkurugenzi Mtendaji, Ndg. Neema Lugangira (katikati) na Mwenyekiti wa Kikundi cha Wabunge Vinara wa Lishe, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dunstan Kitandula (kulia).

Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kushoto) akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi ya Agri Thamani Foundation, Mhe. Mizengo Pinda alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)