Barcelona yapunguzwa kasi La Liga


Walinzi wa Barcelona wakielekea katikati kinyonge baada ya Alexander Isak kuisawazishia Real Sociedad dakika ya 62 katika sare ya 2-2 leo Uwanja wa Reale Arena mjini Donostia-San Sebastian.

 Bao la kwanza la Real Sociedad limefungwa na Mikel Oyarzabal kwa penalti dakika ya 12, wakati ya Barca yamefungwa na Antoine Griezmann dakika ya 38 na Luis Suarez dakika ya 49.