Shirika la Reli mbioni kuongeza safari treni ya abiria Dar-Moshi


Shirika la Reli Tanzania (TRC) limesema lipo mbioni kuongeza safari za treni ya abiria kati ya Dar es Salaam na Moshi kutoka mbili kwa wiki hadi tatu.

Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo, Masanja Kadogosa ameyasema hayo katika mkutano wake na waandishi wa habari wakati akizungumzia utendaji wa shirika hilo tangu mwaka 2015.

Amesema Watanzania wamepokea kwa shauku treni hiyo, kwamba kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka wamepata maoni mengi kuhusu kuongezwa kwa safari hizo.

“Hii ni treni ya Watanzania wametoa maoni na tumeyapokea tumeyafanyia kazi, tutaona ni jinsi gani tunajipanga kuhakikisha inakwenda Moshi mara tatu kwa wiki na kurudi Dar mara tatu,”

Kadogosa pia amezungumzia ukarabati wa mabehewa ya shirika hilo na kueleza kuwa wana nia ya kuyafufua na kuyaweka katika hali nzuri ili yatumike.

Kwa sasa treni hiyo inatoka Dar es Salaam kila Ijumaa na Jumanne na Moshi kila Jumatano na Jumamosi.