Na Amiri kilagalila-Njombe
Jeshi la Polisi Mkoani Njombe linamshikilia mkazi mmoja wa mtaa wa Joshoni Halmashauri ya Mji Njombe , Hezron Ndone (44) kwa tuhuma za kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtoto wake mwenye umri wa miaka 11,ambayo yalikuwa yakilalamikiwa na mke wake kwa mda mrefu mpaka wananchi walipopaza sauti juu ya tukio hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Hamisi Issa amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo, Hezron Ndone ambaye ni mfanyabiashara wa mkaa na kusema pindi taratibu zitakapokamilika atafikishwa mahakamani.
“Katika hali isiyokuwa ya kawaida baba huyu ametumia mbinu zake chafu kumuamisha mkewe kwenye chumba chake na kumpeleka chumba kingine na akaamua kumchukua mwanae na kukaa naye kwenye chumba chake,na matokeo yake imetokea madhara, na baba huyu tunamshilia kwa kuwa na mahusiano kati yake na mtoto wake ambayo yalikuwa yanalalamikiwa na mama mtu kila mara mpaka wananchi wamepaza sauti na jeshi lilienda kuhakikisha jambo hili limekuwa ni mgogoro katika familia”alisema kamanda Hamisi Issa