Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Msanii Hodari wa Miondoko ya Hip Hop nchini Fareed Kubanda (Fid Q) anatarajia kufanya show ya kali ya kimataifa katika Tamasha la sanaa la Kimataifa la KAN Ferstival litakalofanyika eneo la Usa River ambapo tamasha hilo litaanza january 22 hadi 25 mwaka huu.
Mkurugenzi wa sanaa katika Tamasha hilo Dave Ojay amesema kuwa Tamasha hilo linalenga kuhamasisha sanaa ya Kiafrika ,Utamaduni wa Kiafrika ambapo Wasanii mbalimbali watatumbuiza akiwemo Msanii Mahiri Fid Q.
Licha ya Msanii huyo kuwepo kutakua na wasanii wa Isabella Novella kutoka Msumbiji ,Tear Drop kutoka Kenya,na Victor Kunonga kutoka Zimbabwe pamoja na Wachekeshaji na Live Band.
Mkurugenzi wa Programu katika kituo cha Mafunzo ya Uongozi ambacho ni cha Ushirikiano wa Denmark na Tanzania (MS-TCDC) MSTDC ,Sara Ezra Teri hi limelenga katika kusaidia kubadilishana ujuzi mbalimbali ikiwemo sanaa pia kuwaelimisha vijana , pia jinsi ya kuzikabili changamoto mbalimbali ikiwemo mimba za utoto,ukosefu wa ajira,rushwa na ufisadi.
Sara amewataka vijana kujitokea kwa wingi katika Tamasha hilo na kutumia fursa za mafunzo yanayotolewa na kituo hicho katika kujiendeleza kielimu.