Makonda ataka muda wa kufanya kazi NIDA uongezwe

Mkuu wa Mkoa wa DSM Paul Makonda jana amewaelekeza NIDA kuongeza muda wa kufanya kazi hadi saa kumi na mbili jioni ndani ya siku zote saba za wiki huku pia akisema vituo vimeongezwa ili kuhakikisha Watu wengi zaidi wanapata huduma na waweze kuwahi kusajili laini zao kwa alama za vidole.

"Tunaongeza Watumishi ili kuhakikisha zoezi linakwenda vizuri, Watu wanaofika kwenye kituo wapewe namba na wahudumiwe siku hiyohiyo waondoke"- RC MAKONDA