Dkt. Mwakyembe apokea ujumbe wa wadau wa michezo toka nchini Misri

 Kiongozi wa ujumbe toka nchini Misri akifafanua jambo kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) wakati ujumbe huo ulipomtembelea Waziri Mwakyembe katika ofisi ndogo jijini Dar es Salaam mapema hii leo na kujadiliana masuala mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya michezo ikiwemo la ujenzi wa eneo changamani la michezo.

 Balozi wa Misri nchini, Mhe. Gaber Mohamed Abulwafa akifafanua jambo kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) wakati walipomtembelea Waziri na ujumbe toka nchini Misri na kujadiliana masuala mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya michezo ikiwemo la ujenzi wa eneo changamani la michezo.

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe toka nchini Misri na wadau wa michezo nchini wakati walipomtembelea leo 25 Februari 2020 katika ofisi ndogo za jijini Dar es Salaam na kujadiliana masuala mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya michezo ikiwemo la ujenzi wa eneo changamani la michezo.

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akielekeza jambo kwa ujumbe toka nchini Misri wakati walipomtembelea leo 25 Februari 2020 katika ofisi ndogo za jijini Dar es Salaam na kujadiliana masuala mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya michezo ikiwemo la ujenzi wa eneo changamani la michezo.

Balozi wa Misri nchini, Mhe. Gaber Mohamed Abulwafa (kushoto)akifafanua jambo kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe wakati walipomtembelea Waziri na ujumbe toka nchini Misri na kujadiliana masuala mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya michezo ikiwemo la ujenzi wa eneo changamani la michezo.