"Maisha yangu yote sijawahi kudanga hata wigi hili nimevaa kwa hela yangu na hela ya mashabiki, huwa najisikia vibaya nikimkuta mtoto wa kike anauza mwili au anadanga, niwaambie tunajidhalilisha sana, hatuwawekei maisha mazuri watoto wetu" amesema Isha Mashauzi.
Aidha msanii huyo ameongeza kusema "Mimi ni mwanamke wa kwanza kuimba Taarab, kumiliki bendi, na ndiyo wa kwanza kumiliki gari kwa hela yangu mwenyewe na wala sikwenda Chuo Kikuu bali huwa napita kama njia".