Simba kubadili nembo yake

Klabu ya soka ya Simba imeeleza nia yake ya kutaka kubadili nembo ya klabu hiyo.

Simba ambayo imekuwa ikitumia nembo yenye rangi mbili kuu, nyekundu na nyeupe kwa muda mrefu, imesema kuwa kabla ya kuanza mchakato huo inahitaji kupata maoni mbalimbali ya mashabiki na wadau wa klabu hiyo.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Simba imeweka taarifa hiyo huku ikihitaji mashabiki wake kutuma maoni yao juu ya mabadiliko ya nembo hiyo katika email maalum.