Watu 31 wameuawa katika shambulizi dhidi ya kijiji cha Odossagou nchini Mali.
Shambulizi dhidi ya kijiji kimoja ambacho kimetajwa kuwa wakazi wengi ambao ni kabila la Fulani Odossagou nchini Mali limepelekea vifo vya watu 31.
Waziri mkuu wa Mali kupitia kurasa zake katika mitandoa ya kijamii amesema kwamba idadi ya watu waliofariki katika shambulizi hilo lililoendeshwa dhidi ya kijiji hicho imeongezeka na kufikia watu 31.
Tangazo hilo limefahamisha pia kuwa operesheni za jeshi dhidi ya makundi ya wahalifu zimeanza.
Taarifa zimefahamisha kwamba watu 48 wmefariki wakiwemo wanawake wajawazito watano katika vijiji tofauti nchini Mali.