Waziri wa ulinzi wa Uturuki, Hulusi Akar, akiwa na mkuu wa majeshi Jenerali Yaşar Güler pamoja na mkuu wa vikosi vya nchi kavu Jenerali Ümit Dündar kwa pamoja wamekagua vikosi vya majeshi ya Uturuki vilivyopo mpakani mwa Syria.
Katika uwanja wa ndege wa Hatay walipokelewa na kamanda wa vikosi hivyo Sinan Yayla na viongozi wengine. Akar na viongozi wengine wa jeshi wapo katika ukaguzi wa vikosi vya jeshi.