Kenya: Wangonjwa wa Corona wafikia 15

Kenya imeripoti wagonjwa wapya wanane wenye maambukizi ya virusi vya corona na sasa wamefikia 15 na wengine 368 waliokutana na wagonjwa hao wanafuatiliwa. Kati yao watano ni Wakenya, wawili Wafaransa na mmoja ni wa Mexico

Katibu wa Baraza la Mawaziri la Afya Mutahi Kagwe alisema wagonjwa hao, ambao wamejumuisha Wakenya watano, raia wawili wa Ufaransa na Mmerekani, wametengwa

Kagwe ameongeza kuwa ndege zote za kimataifa zimezuiwa kuingia nchini humo  kuanzia  Machi 25 isipokuwa ndege za kubeba mizigo, ambazo wafanyakazi wake lazima wafuate miongozo madhubuti ya usalama.