Mtuhumiwa wa shambulizi dhidi ya waislamu New Zealand akiri kosa


Mtuhumiwa wa shambulizi dhidi ya waislamu  katika mskiti nchini New Zealand akiri kosa  mahakamani.

Mtu alieendesha shambulizi  dhidi ya mskiti  katika jimbo la Christchurch nchini New Zealand  mwaka  2019 afikishwa mahakamani na kukiri  kosa.

Brenton Tarrant  alishambuliai mskiti na kuwaua watu 51 waliokuwa wakisubiri kufanya ibada Machi mwaka  2019.
Mshtakiwa huyo amekiri makosa yote  aliosomewa na mahakama.

Waziri Mkuu  Jacinda Ardern na jamii ya Waislamu nchini New Zealand wamefurahishwa na kitendo hicho, na hivyo kuruhusu mahakama kuendelea na kesi hiyo hasa kuchukua uamuzi dhidi ya Tarrant.

Muuaji huyo, mwenye umri wa miaka 29 amekiri makosa yanayomkabili bila kushinikizwa na mtu .