https://monetag.com/?ref_id=TTIb Sumaye Akabidhiwa Rasmi Kadi Ya Uanachama CCM | Muungwana BLOG

Sumaye Akabidhiwa Rasmi Kadi Ya Uanachama CCM

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Dkt BASHIRU ALLY leo  Machi 29,2020 amemkabidhi rasmi kadi ya uanachama wa chama hicho Waziri mkuu mstaafu FREDRICK SUMAYE huku akiahidi kufanya sherehe ya kumpokea mwanachama huyo mara baada ya tishio la Virusi vya Corona litakapoisha.

Makabidhiano hayo yamefanyika jijini Dodoma ambapo amesema siku zote chama kinapopokea mwanachama mpya kinafanya sherehe lakini kutokana na uwepo wa virusi hivyo wamesitisha sherehe hiyo kwa sasa.

 Amesema SUMAYE amekabidhiwa kadi Dodoma kwa sababu Chama hicho ni chama cha kitaifa nasio chama cha watu.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa kadi SUMAYE amesema amefurahi amerudi rasmi kwenye chama chake na sasa ni mwanachama kamili.

Amesema wakati anaondoka CCM alisema anaondoka akiwa hana chuki na chama,hana chuki na aliyekuwa mwenyekiti wa CCM wakati huo dokta JAKAYA KIKWETE na hana chuki na mgombea aliyeteuliwa wakati huo dokta JOHN MAGUFULI 

Kwa upande wake Waziri Mkuu Mstaafu ambaye pia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM MIZENGO PINDA amesema amefurahi kwa kuwa wakati wanaondoka CCM alipata shida sana.