Mkuu wa Shirika la Afya Ulimenguni WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus atatoa ujumbe katika mazungumzo hayo, ambapo anatarajiwa kuomba msaada wa kuwezesha utengenezwaji wa vifaa vya kujilinda dhidi ya maambuki ya virusi vya corona, ambavyo vimeadimika.
Katika mkutano na waandishi wa habari jana mjini Geneva, Ghebreyesus alisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kimataifa, katika kupambana na janga la virusi hivyo.
Virusi hivyo vimekwishawauwa watu zaidi ya 21,000 miongoni mwa 471,000
waliokwishaambukizwa kote duniani.
Mapema wiki hii, mawaziri wa fedha na wakuu wa benki kuu kutoka nchi hizo, waliweka mkakati wa kudhibiti virusi hivyo, lakini hawakutoa maelezo zaidi.