Watu milioni moja ulimwenguni waathirika na virusi vya corona tangu kuanza kwake Wuhan China.
Idadi
ya watu walioathirika na virusi vya corona ulimwenguni yaripotiwa
kuongezeka na kufikia watu milioni moja huku idadi ya watu ambao
wamekwishafariki ikiripotiwa kuwa watu 51000.
Nchini Italia idadi ya vifo bado inaripotiwa kuzidi kuongezeka, katika kipindi cha masaa 24 watu 760 wameripotiwa kufariki.
Idadi hiyo pia imepelekea idadi ya watu waliofariki tangu kuanza kwa janga hilo imefikia watu 13915.
Ursula
von der Leyen, mkurugenzi mkuu wa kamishna wa Ulaya amesema kuwa
Italia ndio taifa ambalo lilikuwa limaethirika kwa kiasi kikubwa kwa
idadi ya watu wengi waliofariki kwa virusi vya corona baada ya China.
Ursula
von der Leyen amesema kuwa kulikuwa na umuhimu wa ıushirkiano katika
kipindi hiki kigumu, hali haikuwa jambo rahisi kwa kuwa kila taifa
tayari lilikuwa katika jango la Covid-19.
Nchini Ufaransa watu 471 wamefariki katika kipindi cha masaa 24 na idadi ya vifo inaendelea kuongezeka na kufikia watu 4503.
Nchini Marekani watu 5151 wamekwishafariki .