Shirikisho la soka Ulaya UEFA limeipiga faini club ya Man City ya
England kiasi cha Euro 3000 (Tsh milioni 7.6) kwa kosa la kuvaa jezi za
mazoezi zinazokiuka sheria.
Kosa la Man City walitenda mwezi
uliopita katika mchezo wa UEFA Champions League dhidi ya Real Madrid,
Man City wakati wa warm up kabla ya mchezo jezi zao za warm up walizovaa
logo ya mdhamini iliyokuwepo ilikuwa kubwa zaidi na kukiuka sheria za
mashindano.
Kwa kawaida kuna kiwango cha ukubwa wa Logo inayotakiwa kukaa kwenye
jezi lakini Man City waliweka kubwa, UEFA wamewapa Man City siku 90 za
kukata rufaa kama wataona wameonewa, mchezo huo wa 16 bora ulimalizika
Man City ikishinda 2-1.
Sheria za UEFA zinaeleza kuwa ukubwa wa
logo ya mdhamini katika makoti/jezi ya warm up kabla ya mechi au makoti
wanayoingia nayo dakika chache kabla ya mchezo kuanza yanapaswa kuwa na
saizi ya 20cm square na 200cm square kwa sare zingine zisizokuwa za
kuchezea.