Idadi ya waliopona corona Kenya yafikia 553

Wagonjwa 54 wa virusi vya corona wamethibitishwa kupona nchini Kenya , ikiwa ndio idadi kubwa zaidi kutangazwa kwa siku.

Idadi hiyo sasa inafanya waliopona nchini humo kufikia 553.

Hatahivyo taifa hilo limeandikisha wagonjwa 123 zaidi wa virusi vya corona baada ya saa 24 baada ya sampuli 2,112 kuchunguzwa.

Idadi hiyo mpya inaongeza wagonjwa wa virusi hivyo waliothibitishwa nchini humo kufikia 2,216.

Jumla ya sampuli 85,058 zimefanyiwa vipimo kufikia sasa .

Naibu waziri wa Afya Rashid Aman akizungumza na vyombo vya habari , amesema kwamba Nairobi ilikuwa na wagonjwa 44 , Mombasa ikithibitisha wagonjwa 34, Busia 20 na Uasin Gishu 12.

Wagonjwa wapya pia walirekodiwa katika wilaya za Kajiado -3 ,Kiambu -3, Nyeri -3, Kilifi -2, Garissa na Laikipia zikiwa na wagonjwa mmoja mmoja .

Dkt. Aman alitangaza kwamba watu watatu walifariki kutokana na ugonjwa huo na hivyobasi kufanya idadi ya waliofariki kufikia 74.

Kijana wa miaka 12 ni miongoni mwa wale waliofariki.