Maandamano kupinga ubaguzi na mauaji ya Floyd na Adama Traore nchini Ufaransa

Maandamano  kukemea matumizi ya nguvu ya jeshi la Polisi , kifo cha Adama Traore na George Floyd  yafanyika nchini Ufaransa.

Adama Traore ni kijana mfaransa mwenye asili ya Afrika ambae alifariki  mikononi mwa polisi mwaka  2016 nchini Ufaransa.

Traore alikuwa akiwa na umri wa miaka  24, maandamano yamefanyika nchini Ufaransa pia kukemea mauaji ya George Floyd nchini Marekani.

Licha ya marufuku ya kuandamana mjini Paris, waandamanaji wamemiminika mabarabarani  karibu na karsi ya sheria wakidai haki itendeke kwa watu wote wakikemea mauaji ambayo husababishwa na matumizi ya nguvu ya  maafisa wa jeshi la Polisi.

Wanafamilia ya Adama Traore wameomba haki itendeke kufuatia kifo cha mwanafamilia wao.

Jeshi la Polisi limekabiliana na  waandamanaji takribani 20 000 ambao ilijaribu kuwasamabaratisha  kwa kutumia mabomu ya kusababishwa kutokwa na machozi.

Baada ya waandamanaji waliokuwa wakiandamana wakiwa na mabango  ambayo yameandikwa "haki itendeke kwa Adama Traore" wamekwnda hadi mbele ya ubalozi wa Marekani .

Mbele ya ubalozi huo wa Marekani,  waandamanaji  wamekemea mauaji ya George Floyd yaliotokea wiki ilipita nchini Marekani na kuendelea kwa maandamano.

Tangu Mei  25, maandamano hufanyika nchini Marekani kukemea mauaji ya mmarekani huyo mweusi aliofariki mikononi mwa  maafisa wa usalama  Minneapolis.
Maandamano hayo yamefuatiwa na ghasia na uporaji wa mali na uharibifu.

Kifo cha Adama Traore nchin Ufaransa kilitokea mwaka  2016 , kifo hicho kimefananishwa na matukio ya sasa nchini Marekani.

Ripoti iliotolewa  kuhusu kifo cha Adama Traore  imefahamisha kuwa kijana huyo alifariki kutokana na  matumizi ya nguvu  ya maafisa wa jeshi la Polisi ddhidi yake na alifariki ndani ya gari la Polisi alipokuw akipelkwa hospitali.

Kesi kuhusu tukio hilo nchini Ufaransa bado haijafunguliwa .