Namna sahihi za kukabiliana na changamoto za kimafanikio katika maisha

Nafahamu ya kuwa kila mmoja wetu anahitaji mafanikio makubwa sana kwa kile anchokifanya siku zote, ila tatizo  kuna baadhi  changamoto mbalimbali zinasomsonga na kufanya eidha kefeli kabisa kwa jambo anolifanya au kufanikiwa kwa asilimia chache tofauti na alizokuwa anategemea mwanzoni mwa kuanza jambo.

Kuna wakati mwingine tunajikuta tunakata tamaa baada ya kuona baadhi ya changamoto zinatokea na kuzuia mafanikio ambayo tumejipangia. Changamoto hizi zinaweza zikajitokeza katika biashara, elimu, kazi kwa mfano kufukuzwa kazi ambayo ulikuwa unaitegemea, kufiwa na mtu ambaye ulikuwa unamtegemea na changamoto zinginezo.

Pia kuna wakati mwingine changamoto zikitokea tulio wengi  hukataa tamaa na muda mwingine na kujiona  hutafai kuendelea kuishi ,pia wakati mwingine huwa hata tunakufuru kwa kusema baadhi ya maneno kama vile Mungu kampendelea na mengineyo mengi.

Lakini ndugu msomaji wa makala hii tukumbuke ya siku zote changamoto ni njia ya kufikia mafanikio tunayoyahitaji. Pia changamoto hutokea ili kupima imani yako je wewe ni mtu wa aina gani katika kakabilana na changamoto?

Zifutato ni baadhi ya njia ya jinsi ya kukabilaiana na changamoto.

Kubali changamoto zinajitokeza.
Kama nilivyoeleza hapo awali ya kwamba changamoto ni lazima zitokee katika safari yako ya mafanikio, hivyo basi hakikisha ya kwamba unakua ni mtu kwa kuzikubali  changamoto hizo na ujue ni jinsi gani unaweza kupambana nazo ili uweze kutimiza malengo yako, mfano huenda ukawa unafanya biashara mahali fulani ila mwanzoni mwa biashara yako wateja walikuwa wengi ila kwa sasa wamepungua jaribu kufanya taathimini juu hili uone ni sababu zipi zilizochangia kutokea kwa hili na siyokuwa  ni mtu wa kukataa taamaa maana hakuna dhambi kubwa kama kukaata tama.

Tafuta washauri
Nafahamu ya kuwa baadhi yetu huwa tuna watu wa karibu ambao huwa tunaweelezea shida zetu ili kupata ushauri. Mfano wa  watu wa karibu wanaweza kuwa ndugu, marafiki na watu wengine. Pia unaweza kuwatumia viongozi wa dini kwa jambo linalolokukatiza kwani ni watu ambao ni washauri wazuri kwa  jambo linalokukatiza  na kukuzuia kukamilisha malengo yako.

Pia katika utautizi wa changamoto watu wengi huwa tunakosea sana. Huwa tunaangalia effect (madhara) ya jambo fulani kutokea badala ya kualia causes (sababu) ya jambo Fulani kutokea. Huenda ukawa hujanielewa ngoja nikupe mfano ufutao; katika baadhi ya maeneo hapa nchini kuna ugonjwa wa mlipuko ambao umetokea unaitwa kipundupindu lakini katika utatutizi juu ya ugonjwa huu watu huenda kuatibu madhara (effects) sawa ni jambo nzuri lakini ni vyema kuanza kuangalia ni nini chanzo (causes) cha ugonjwa huu kutokea ndipo tuje tuangalie madhara (effect).

Ukifuata kanunu hii ya kuangalia chanzo yaani (causes)  harafu uje kuangalia effect (madhara) itasaidia kupunguza changamoto zingine zinazokutatiza katika kufanikisha malengo yako.

Mwisho naomba nimalize kwa kusema ”usizibe ufa kabla ya kujua chanzo cha ufa kutokea’’

Na. Benson Chonya.