Rais Magufuli atajwa kati ya watu 10 walioleta mabadiliko Afrika

Utendaji kazi wa Rais John Pombe Magufuli unaendelea kuonekana nje ya mipaka , baada ya Jarida kubwa la African Report kumtaja Kama miongoni mwa watu 10 walioleta mabadiliko makubwa barani Afrika

Jarida hilo limemtaja Rais Magufuli kama kiongozi aliyeweza kufanya mapinduzi makubwa katika miradi ya Kiuchumi na kijamii , na kusababisha uchumi wa Tanzania kua ni uchumi unaokua kwa kasi zaidi barani Afrika

Pia limemuelezea Rais Magufuli Kama kiongozi aliyeweza kurejesha nidhamu ya kazi kwa viongozi wa umma, kudhibiti rushwa na Kupunguza matumizi mabaya ya kodi za wananchi

Vilevile limesifia juhudi zake za kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji nchini Tanzania, pamoja na kujitolea kupunguza mshahara wake kipindi alipoingia madarakani.