Vurugu na vifo nchini Afghanistan

Raia 23 wamepoteza maisha kwenye matukio tofauti ya vurugu za Taliban katika wiki iliyopita nchini Afghanistan.

Katika taarifa iliyotolewa na Baraza la Usalama la Taifa nchini humo, raia 23 waliuawa na wanamgambo wa Taliban katika ghasia ndani ya majimbo 16 ya nchi hiyo wiki iliyopita.

Uhalifu uliosababishwa na wanamgambo wa Taliban umepelekea watu wengine 45 kujeruhiwa.

Hakuna maelezo yoyote ambayo yametolewa kutoka kwa Taliban wenyewe kuhusiana na taarifa hiyo.