CHADEMA yampitisha Tundu Lissu kuwa mgombea Urais wa Tanzania

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimempitisha mwanasiasa Tundu Lissu kuwa mgombea Urais wa Tanzania katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 28 mwaka huu.

Jumla ya wapiga kura ambao ni wajumbe wa Baraza Kuu - 442, Idadi ya kura zilizoharibika - 0, Idadi ya kura halali - 442

1. Tundu Antipas Lissu - 405
2. Lazaro Samuel Nyalandu - 36
3. Dkt. Mayrose Kavura Majinge - 1