Camera zamnasa Mbunge akitazama picha za ngono Bungeni

 


Mbunge wa Jimbo la Chonburi Thailand Ronnathep Anuwat amezua gumzo mitandaoni na mitaani nchini humo baada ya camera za Bunge kumnasa akiwa anatazama picha za ngono kwenye simu yake wakati Bunge la Bajeti likiendelea.

Picha moja inamuonesha Mwanamke akiwa uchi wa mnyama na nyingine Mwanamke yupo kifua wazi, Mbunge huyo amekiri kutazama picha hizo na kusema alikuwa anafanya upembuzi yakinifu >"nilikuwa nakagua kama picha ni feki au Original, pia kuangalia kama Wanawake walipiga picha hizi kwa hiari au walilazimishwa wakiwa mazingira hatari ili niwasaidie kupata haki, ndio maana nilivua na mask ili nione vizuri"

Spika wa Bunge hilo amesema hayo ni mambo binafsi na kusisitiza kamwe hawezi kuingilia faragha wala starehe za Mbunge ambazo haziharibu kazi za Kibunge.

Post a Comment

0 Comments