Mchezaji tenisi wa Japan awashukuru mababu zake kwa ushindi


Mchezaji filamu maarufu wa Japan Naomi ambaye amefanikiwa kushdna shindano la US Open mwishoni mwa Juma, amewashangaza wengi baada ya kuwashukuru mababu zake kwa ushindi huo.

"Ningependa kuwashukuru mababu zangu kwasababu kila wakati, ninapokumbuka kuwa damu yao inapita katika mishapa yangu inanikumbusha kuwa siwezi kushindwa ," nyota huyo alituma ujumbe huo kupitia ukurasa wake wa Jumapili.

Katika kila mechi katika shindano la mwaka huu la US open, Osaka alivalia barakoa yenye jina la mhanga mweusi wa ghasia zinazodaiwa kufanywa na polisi au za ubaguzi wa rangi nchini Marekani.

Jumamosi alivaa barakoa yenye jina la Tamir Rice, aliyeuliwa na polisi kwa risasi katika eneo la Cleveland akiwa na umri wa miaka 12 mwaka 2014.

"Ninahisi kuwa ni wakati wa kuwafanya watu kuanza kuongea," alisema Osaka, mwenye umri wa 22, ambaye anaishi Marekani, lakini anachezea timu ya Japan.

Inadaiwa kua binafsi Osaka amekuwa akikumbwa na ubaguzi wa rangi.

Post a Comment

0 Comments