Serikali ya Ufaransa yakemea shinikizo za polisi dhidi ya wahamiaji katika mjini Paris


Waziri ya Mambo ya Ndani wa Ufaransa Gerald Darmanin, amesema kuwa uchunguzi umeanzishwa juu ya shinikizo za polisi dhidi ya wahamiaji waliofukuzwa kutoka kwenye kambi zao hapo jana  katika mji mkuu Paris. 

Darmanin alitoa maelezo kwenye Twitter na kusema kuwa aliwasilishiwa ripoti kuhusiana na shinikizo za polisi dhidi ya wahamiaji wapatao 500 ambao wengi wao ni raia wa Afghanistan waliokita kambi katika eneo la Republique Square. 

Darmanin alisisitiza kuwa harakati hizo zilizotekelezwa na polisi wanaohusiana na vikosi vya kitaifa vya IGPN haziwezi kukubalika na kusema, 

"Nimeipa IGPN masaa 48 kutoa tamko kwa umma na kujitetea." 

Darmanin pia alisema kuwa picha za polisi zilizochapishwa na kuwaonyesha walivyokuwa wakiharibu kambi za wahamiaji ni za kustaajabisha. 

Kwa upande mwingine, picha zilizochapishwa na vyombo vya habari zilizowaonyesha polisi wakitumia vitoa machozi kwenye makabiliano na wahamiaji, zilizuwa mjadala mitandaoni. 

Katibu mkuu wa shirikisho la wanahabari wa jumuiya ya Ulaya iliyokuwa na makao makuu yake Brussels na kujumuisha wanahabari zaidi ya 320,000 kutoka nchi 45, pia alikemea vikali shinikizo za polisi. 

Gutierez alibainisha kutekelezwa kwa visa 3 vya shinikizo vilivyonaswa kwa kamera iliyofungwa kwa polisi mmoja na kusema,

"Waziri wa Mambo ya Ndani amechochea shinikizo za polisi kutokana na sera za kutowachukuliwa hatua. Darmanin anapaswa kujiuzulu." 

Wanahabari wengine wengi pamoja wanaharakati waliwaunga mkono wahamiaji na kukekemea vikali matukio hayo. 

Post a Comment

0 Comments