https://monetag.com/?ref_id=TTIb Vanessa Mdee aibukia kwenye wimbo wa Rotimi | Muungwana BLOG

Vanessa Mdee aibukia kwenye wimbo wa Rotimi


Miezi mitatu tangu mwanamuziki wa Tanzania, Vanessa Mdee kutangaza kuachana na muziki, ameibuka kwenye wimbo mpya wa mpenzi wake,  Rotimi alioutoa leo Jumanne Desemba mosi, 2020.


Katika video ya wimbo huo wa mapenzi unaoitwa Love Someday, Vanessa ameigiza kama mpenzi wa Rotimi.


Wimbo huo umetoka kwenye kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Rotimi ambaye kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram, mwanamuziki huyo anayeishi Marekani, amesema wimbo huo ni kwa ajili ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa pamoja na Vanessa.

Post a Comment

0 Comments