TIMU ya AZAM FC inatarajia kucheza leo uwanja wa Aman mjini Unguja dhidi ya
Mlandege FC katika mashindano ya kombe la Mapinduzi.
Katika mashindano hayo timu ya Simba SC inatarajia kucheza kesho dhidi
ya Chipukizi saa 10 jioni huku Yanga FC ikicheza na Namungo saa
mbili usiku.
Timu ya Mtibwa Sugar ambao ni mabingwa watetezi wa mashindano hayo
ya kombe la Mapinduzi imeanza vyema jitihada zake za kutwaa tena kombe hilo
baada ya juzi kuifunga Chipukizi bao 1-0 ndani ya dakika 57.
Mchezo huo ulichezwa kwenye dimba la Amaan majira ya saa 10:00 jioni ambao
ulihudhuriwa na mashabiki kiasi ambapo licha ya kushinda mechi hiyo Mtibwa
wilipata upinzani mkali kutoka kwa timu ya Chipukizi.
Timu hizo zilikianza kipindi cha kwanza kwa kushambuliana kwa zamu kila
mmoja akisaka bao la kuongoza, lakini hadi kipindi cha kwanza kinamalizika
hakuna timu iliyoweza kuona lango la mwezake.
Katika kipindi cha pili timu ya Mtibwa Sugar ilianza kulishambulia lango
la Chipukizi huku ikifanya mabadiliko ya kumtoa Salum Kanoni na kumuingiza
Ibrahim Hilika dakika ya 54.
Mabadiliko hayo yalileta neema kwa Mtibwa ambapo dakika ya 57 Mtibwa
ilijipatia bao hilo pekee lililotiwa kimiani na Ibrahim Hilika.
Katika dakika ya 60 timu ya Chipukizi nayo ilifanya mabadiliko kwa kumtoa
mchezaji Ali Khamis na kumuingiza Mundhir Iman, ili kuongeza kasi ya
mashambulizi kwa kutafuta bao la kusawazisha lakini walishindwa kutumia
nafasi walizozipata.
0 Comments