Idadi ya vifo vya wanajeshi walioshambuliwa Mali yaongezeka

Idadi ya wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa (UN) waliofariki kwenye shambulizi la kigaidi lililoendeshwa katika mkoa wa Timbuktu nchini Mali imeongezeka hadi 4.

Katika taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Idara Kuu ya Usalama wa Umma nchini Ivory Coast, iliarifiwa kwamba wanajeshi wa kulinda amani wa UN walioshambuliwa walikuwa raia wa Ivory Coast na mmoja wao aliyekuwa amejeruhiwa alifariki.

Katika shambulizi hilo lililofanyika hapo jana katika eneo la Timbuktu-Douentza, bomu lilitegwa barabarani na kulipuka wakati wa gari lililokuwa limebeba wanajeshi wa UN likipita, na baadaye likashambuliwa kwa risasi.

Kulingana na taarifa za awali, ilitangazwa kuwa wanajeshi 3 wa kulinda amani wa UN walipoteza maisha.

 

Post a Comment

0 Comments