https://monetag.com/?ref_id=TTIb Kampuni kubwa zasitisha ufadhili wake kwa chama cha Republican | Muungwana BLOG

Kampuni kubwa zasitisha ufadhili wake kwa chama cha Republican

 Baadhi ya wanasiasa wa Republican tayari wameanza kuhisi athari ya vurugu vya Januari 6 ambapo wafuasi wa Trump walivamia bunge.



Zaidi ya makampuni 20 ya Marekani yametangaza kusitisisha ufadhili wao kwa kampeni za chama cha Republican hasa kwa wabunge wa chama hicho waliopinga ushindi wa mgombea wa Democratic Joe Biden.


Ghasia zilitokea wakati wa kikao maalumu katika mabunge yote mawili cha kuidhinisha kura za wajumbe ambacho kilikatizwa na uvamizi wa eneo la Capitol kulikotekelezwa na wafuasi wa Trump waliozua vurugu.


Lakini baada ya kikao hicho kilichovurugwa kurejelewa tena, zaidi ya wabunge 100 wa bunge la Wawakilishi kadhaa, wengi wao wakiwa kutoka chama cha Republican ambao walikuwa wanapinga matokeo hayo, wabadilisha msimamo wao.



Post a Comment

0 Comments