Ashtakiwa kwa 'kumuua na kumla mama yake'


Mtu mmoja ameshtakiwa nchini Uhispania kwa tuhuma za kumuua mamake, kisha kuukata vipande mwili wake na kuula.

Alberto Sanchez Gomez alikamatwa mwaka 2019 baada ya maafisa wa polisi kwenda katika nyumba ya mamake mwenye umri wa miaka 66 kutokana na wasiwasi wa rafiki mmoja.

Maafisa wa polisi wanasema kwamba walipata vipande vya mwili vilivyotapakaa ndani ya nyumba hiyo, huku vingine vikiwa vimehifadhiwa katika ndoo ya plastiki.

Mshukiwa ameambia mahakama kwamba hakumbuki kuukatakata mwili na kumla mamake.

Amedaiwa kuugua tatizo la kiakili pamoja na tumiaji wa mihadarati kabla ya kukamatwa kwake.

Vyombo vya habari vya Uhispania vinasema kwamba bwana huyo alikuwa nafahamika na maafisa wa polisi kwa kumfanyia ghasia mamake , Maria Soledad Gomez, mara kwa mara na kwamba alikiuka agizo la mahakama la kukaa mbali na mzazi wake huyo wakati wa kukamatwa kwake.

Mahakama ilielezewa kuhusu tukio ambalo maafisa wa polisi walikutana nalo katika nyumba hiyo mashariki mwa Madrid mnamo Februari 2019.

Baadhi ya mabaki yake yalikuwa katika hali ya kutaka kupikwa na mengine kuhifadhiwa, linaripoti gazeti la El Mundo.

Mshukiwa aliyekuwa na umri wa miaka 26 wakati huo, alikiri kumnyonga mamake na kusema kwamba mara nyengine alikula vipande vya mwili huo na mara nyenagine akawapatia mbwa.

Post a Comment

0 Comments