https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mawakili wa Zuma wajiondoa katika uwakilishi wake kabla ya kesi ya ufisadi kuanza | Muungwana BLOG

Mawakili wa Zuma wajiondoa katika uwakilishi wake kabla ya kesi ya ufisadi kuanza

 


Bwana Zuma anakana mashiotaka yote dhidi yakeImage caption: Bwana Zuma anakana mashiotaka yote dhidi yake

Mawakili wa rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma wamewasilisha waraka wa kujiondoa katika uwakilishi wake.

Mawakili hao hawakutoa sababu ya kufanya hivyo.

Waraka huo uliwasilishwa Jumatano kufuatia hukumu ya wiki iliyopita ambapo rais huyo wa zamani alishindwa katika kesi ya rufaa dhidi ya azma ya taifa ya kutaka kupata pesa ambazo lilimgarimia kisheria Bw Zuma.

Hii inakuja kabla ya kuanza kwa kesi ya ufisadi inayotarajiwa kuanza tarehe 17 Mei.

Bw Zuma anakabiliwa na mashitaka 16 juu ya dola bilioni $2 (£1.4bn) za mkataba wa taifa wa silaha, ikiwa ni pamoja na wizi, utakatishaji wa pesa - mashitaka ambayo anayakana.

Post a Comment

0 Comments