Rais Samia: Tutaendelea kuilea ATCL kimkakati


Rais Samia amesema kuwa serikali yake itaendelea kulilea shirika la nchi hiyo kimkakati ikiwemu kulitua mzigo wa madeni

Kiongozi huyo amesema ATCL limerithi madeni na hivyo kwa sasa linaonekana kuwa halina thamani na kutengeneza hasara.

"Hatutakubali liendelee kutengeneza hasara baada ya uwekezaji mkubwa uliofanyika...Tunaenda kulifanyia uchambuzi yakinifu na tutawaweka watua ambao wataliongoza ili kutengeneza faida."

Rais Samia pia amesisitiza kuwa serikali inatambua kuwa biashara ya usafiri wa ndege ni ngumu na inajitahidi kuepuka yote ambayo yhayana tija kwa shirika.

Post a Comment

0 Comments